Skip to main content

Featured

Chahilu history in Lulogooli : Gaa kale gaa Chahilu (1942-2025)

Bernard Philimona Chahilu 1942-2025  Liivulwa Mukuluundu Bernard Philemon Chahilu yivulwa muhiga gwa 1942 mweli gwa kavili guvee sita (6/2/1942). Nu mwana wa Elam Kilago na maama Jelida Modani ma vosi vaakuza. Nu muyaayi Mukizuungu Mudidi mwifwa Mumasiingila Muvisonye. Yiivulwa muyaayi munifu mulidaala lye Gaigedi, Gaigedi logongo, Wodanga Lusoma, Sabatia Sub-county, Vihiga County. Kuviikilwa makono. Yaaviikilwa ku makono no mwilwazi Daudi Kadenge muhiga gwa 1942 mulidaala lie Gavudia mulivugaana lia Valina. (Friends Church). Likevwa Yaakevwa muhiga gwa 1952 kekevo chalaangwa Silula. Lisooma Yaataangila lisooma lilie ha Gaigedi masoomo go muluguki. Yaamanya niazya Gahumbwa Primary muhiga gwa 1955 mukilaasi kia kavaga. Yaakola ligela lia vaalaanga C.E.E. (Common Entrance Exam) muhiga gwa 1956 ha Gahumbwa. Muhiga gwa 1957 yaazya kusooma mukilaasi cha kataano ha Kericho Township School. Muhiga gwa 1958 yaazya kusooma ha Kigama Intermediate mukilaasi cha siita niakolela ho ligela liala...

Fainali za mijadala ya shule za msingi - 2

Tumelianza juma la fainali za mashindano yetu ya mijadala. Ijumaa ya tarehe 26 mwezi huu wa Julai ndiyo siku shule nne zitapambana kwenye nusu fainali na kisha fainali ili maktaba ya Saniaga iliyopo Wangulu ipate mshindi wa Mijadala yake, huu ukiwa wa pili tangu tulipoanza kirasmi mashindano ya mijadala. 

Kama ilivyosemwa awali,  mijadala ya maktaba ya Saniaga ina nia ya kukuza na kuendeleza isimu kuu ya jamii kifikra na kivitendo. Wanafunzi na walimu wanahusishwa katika utafiti na uvumbuzi wa mienendo na hulka halisi, kuihaiisha katika maongezi na matumizi, kuieneza na kuikuza kwa minajili ya tuliopo na vizazi vijavyo. 

Kwa jinsi hii mijadala yetu ina mada pime kulingana na mafunzo yanayotokana na kujihusisha kwenye mashindano. Umbali huu tumeweza kuhusisha wanafunzi vilivyo na ni furaha yetu kwamba isimu asili yazidi kupata ufahamu miongoni mwao. 

Wanapokamilisha mada ya Nyimbo za Kale muhula huu wa pili (walivyokamilisha mada ya muhula wa kwanza iliyokuwa kwenye lugha ya kiingereza 'Use of mother tongue as a guiding and counseling tool in primary schools'), twatarajia kwamba mashindano ya mwaka ujao yatakua ya kufana zaidi yakiwa na mada nzito ili kuendelea kukuza isimu kuu yetu. 

Washindi watatuzwa, walimu na wanafunzi. Maktaba ya Saniaga na shirika lote la Saniaga litanufaika pia hivi kwamba malengo yake yanazidi kupata ufanisi na uhusikaji wa jamii ili iendelee katika ustawi wake. Kila mmoja wetu atakua wa furaha. 

Ni hapo basi mwakaribishwa nyote katika mashindano haya, mujionee jinsi wadogo watakao ridhi uzuri wetu (ubaya twauficha) wanavyoelezana kinagaubaga. Njooni mujifahamishe mengi kuhusu Maktaba ya Saniaga. Na muhimu njooni ili tunapotuza washindi na kuhimiza waliokosea kutia bidii wakati ujao, tuone ni vipi tutazidi kutia bidii kwenye malengo mengine ya shirika la kijamii la Saniaga. 

Mwaminifu, 

Comments