Skip to main content

Featured

Luanda Reggae Defenders - what is your long term agenda?

Luanda Reggae Defenders is a now a popular movement with roots in Vihiga and border Siaya and Kakamega counties Attention is brought to the manner and conduct the movement has gained fame and followers, mainly the Youths. The movement capitalizes on funerals. With a poor culture of putting the dead to rest, the Reggae Defenders have taken it by storm and rebranded the infamous ‘Disco Matanga’ – disco at funeral. Reggae Defenders on move. Pic: Charles Rankings: Facebook They mobilize quickly on the day the dead will be discharged from the mortuary. They have this huge old school sound system that is over buzzing to no clear reggae song - that they hire a pickup to carry - and it has a young DJ mainly standing there than mixing anything. Often, against the rules, the casket is grabbed from a hearse vehicle and tied to a motorbike. There it will be swayed and jerk breaked between other motorbikes on the narrow roads. That, is, how a fellow soldier, often a young dead, is mourned. ...

Fainali za mijadala ya shule za msingi - 2

Tumelianza juma la fainali za mashindano yetu ya mijadala. Ijumaa ya tarehe 26 mwezi huu wa Julai ndiyo siku shule nne zitapambana kwenye nusu fainali na kisha fainali ili maktaba ya Saniaga iliyopo Wangulu ipate mshindi wa Mijadala yake, huu ukiwa wa pili tangu tulipoanza kirasmi mashindano ya mijadala. 

Kama ilivyosemwa awali,  mijadala ya maktaba ya Saniaga ina nia ya kukuza na kuendeleza isimu kuu ya jamii kifikra na kivitendo. Wanafunzi na walimu wanahusishwa katika utafiti na uvumbuzi wa mienendo na hulka halisi, kuihaiisha katika maongezi na matumizi, kuieneza na kuikuza kwa minajili ya tuliopo na vizazi vijavyo. 

Kwa jinsi hii mijadala yetu ina mada pime kulingana na mafunzo yanayotokana na kujihusisha kwenye mashindano. Umbali huu tumeweza kuhusisha wanafunzi vilivyo na ni furaha yetu kwamba isimu asili yazidi kupata ufahamu miongoni mwao. 

Wanapokamilisha mada ya Nyimbo za Kale muhula huu wa pili (walivyokamilisha mada ya muhula wa kwanza iliyokuwa kwenye lugha ya kiingereza 'Use of mother tongue as a guiding and counseling tool in primary schools'), twatarajia kwamba mashindano ya mwaka ujao yatakua ya kufana zaidi yakiwa na mada nzito ili kuendelea kukuza isimu kuu yetu. 

Washindi watatuzwa, walimu na wanafunzi. Maktaba ya Saniaga na shirika lote la Saniaga litanufaika pia hivi kwamba malengo yake yanazidi kupata ufanisi na uhusikaji wa jamii ili iendelee katika ustawi wake. Kila mmoja wetu atakua wa furaha. 

Ni hapo basi mwakaribishwa nyote katika mashindano haya, mujionee jinsi wadogo watakao ridhi uzuri wetu (ubaya twauficha) wanavyoelezana kinagaubaga. Njooni mujifahamishe mengi kuhusu Maktaba ya Saniaga. Na muhimu njooni ili tunapotuza washindi na kuhimiza waliokosea kutia bidii wakati ujao, tuone ni vipi tutazidi kutia bidii kwenye malengo mengine ya shirika la kijamii la Saniaga. 

Mwaminifu, 

Comments