Skip to main content

Featured

Heavy responsibilities for elder aunt among the Logooli

With Seenge Fonesi. She is the elder grand daughter of Isagi and elder daughter of Amugasya. She is often present in functions involving the family of Amugasya. Pic taken on 18/4/2024. The elder sister soon becomes the elder aunt. It is this “seenge munene” (elder aunt) tag that she is tied to many cultural responsibilities – back home. To her marital family she may appear as any other woman, but she is not so in the eyes of her people. Marriage does not steal her away as it would happen with other daughters of the old man. To her, as days go and the old man and woman of the estate are dependents, she becomes increasingly present.  Her brothers also need her for almost all traditional markings. They are marrying, she needs to welcome the new wife. They are giving birth, she needs to come to midwife or “bless” the new born. They are paying dowry she needs to lead the women delegate. There is a conflict she needs to come for a hearing.  And many others. Traditions does not expect her to

Fainali za mijadala ya shule za msingi - 2

Tumelianza juma la fainali za mashindano yetu ya mijadala. Ijumaa ya tarehe 26 mwezi huu wa Julai ndiyo siku shule nne zitapambana kwenye nusu fainali na kisha fainali ili maktaba ya Saniaga iliyopo Wangulu ipate mshindi wa Mijadala yake, huu ukiwa wa pili tangu tulipoanza kirasmi mashindano ya mijadala. 

Kama ilivyosemwa awali,  mijadala ya maktaba ya Saniaga ina nia ya kukuza na kuendeleza isimu kuu ya jamii kifikra na kivitendo. Wanafunzi na walimu wanahusishwa katika utafiti na uvumbuzi wa mienendo na hulka halisi, kuihaiisha katika maongezi na matumizi, kuieneza na kuikuza kwa minajili ya tuliopo na vizazi vijavyo. 

Kwa jinsi hii mijadala yetu ina mada pime kulingana na mafunzo yanayotokana na kujihusisha kwenye mashindano. Umbali huu tumeweza kuhusisha wanafunzi vilivyo na ni furaha yetu kwamba isimu asili yazidi kupata ufahamu miongoni mwao. 

Wanapokamilisha mada ya Nyimbo za Kale muhula huu wa pili (walivyokamilisha mada ya muhula wa kwanza iliyokuwa kwenye lugha ya kiingereza 'Use of mother tongue as a guiding and counseling tool in primary schools'), twatarajia kwamba mashindano ya mwaka ujao yatakua ya kufana zaidi yakiwa na mada nzito ili kuendelea kukuza isimu kuu yetu. 

Washindi watatuzwa, walimu na wanafunzi. Maktaba ya Saniaga na shirika lote la Saniaga litanufaika pia hivi kwamba malengo yake yanazidi kupata ufanisi na uhusikaji wa jamii ili iendelee katika ustawi wake. Kila mmoja wetu atakua wa furaha. 

Ni hapo basi mwakaribishwa nyote katika mashindano haya, mujionee jinsi wadogo watakao ridhi uzuri wetu (ubaya twauficha) wanavyoelezana kinagaubaga. Njooni mujifahamishe mengi kuhusu Maktaba ya Saniaga. Na muhimu njooni ili tunapotuza washindi na kuhimiza waliokosea kutia bidii wakati ujao, tuone ni vipi tutazidi kutia bidii kwenye malengo mengine ya shirika la kijamii la Saniaga. 

Mwaminifu, 

Comments